Skip to main content

Jinsi ya Kutengeneza Website – Part 01

Hii ni makala ya kwanza katika mfululizo wa mafunzo ya Jinsi ya Kutengeneza Website. Karibu ujifunze!

Website ni nini?

Kwa Kiswahili tunaita tovuti au wavuti ingawa katika mafunzo haya tumetumia neno website kwani ndio linalofahamika na wengi na hivyo itakuwa rahisi kwa watu kufahamu nini tunakizungumzia.

Website ni mtandao ambao unatengenezwa kwa lengo la kuweka data au taarifa za aina mbalimbali (Usichanganye na Blog ambayo taarifa huwekwa kwa njia ya makala).

 Mtu anaweza kutengeneza Website kwa ajili ya kuweka taarifa za biashara yake katika mfumo wa kurasa, au kutoa elimu au kufundishia.

Website inakuwa na Kurasa ya nyumbani (Homepage) ambayo baada ya mtu kuingiza anuani tu anafikia.

Katika ukurasa wa nyumbani kunawekwa taarifa za msingi kuhusu website na taarifa nyingine huwekwa katika kurasa nyingine ambazo zinaweza kufikika kiurahisi kupitia links zilizowekwa au katika MENU.

 Mifano ya Website ni kama https://necta.go.tz n.k.

 

Katika sehemu hii ya kwanza utajifunza mambo ya muhimu unayotakiwa kufahamu kabla hujaanza kutengeneza Website.

 Usihofu hakuna ugumu wowote!

 

Mambo ya Muhimu Unayotakiwa Kufahamu Kabla Hujaanza Kutengeneza Website.

1.Domain na usajili wake: Domain ni jina au anuani ya website yako ambayo watu wataandika watakapotaka kutembelea katika website yako, mfano www.jina.co.tz  Kuna domain za aina mbalimbali kama .com, .org, .online, .net, .co.tz, .go.tz, na kadhalika. Domain zinasajiliwa katika kampuni mbalimbali zilizopo nchini au hata nje ya nchi. Mfano wa Kampuni zinazotoa huduma hizo kwa Tanzania ni Yatosha, Duhosting, Extreme Web na nyenginezo. Kampuni maarufu ya nje unayoweza kusajili domain ni Godaddy (zipo nyingine pia).

 

2. Hosting: Hii ni huduma ya kurusha website yako hewani, yaani ili website yako iwe mtandaoni na watu waweze kuifikia ni lazima ifanyiwe hosting ambayo inakupatia nafasi ya kuhifadhi taarifa za website yako. Pia huduma ya hosting inakupatia CPANEL(Control Panel) ambayo utaitumia kucontrol website na mafaili yako.

 

3. Ufahamu wa Lugha za kimtandao (codes) angalau HTML na CSS itakuwa vizuri zaidi ukifahamu na Javascript na PHP. Usijali, hii namba tatu sio lazima hata kama haujui chochote kati ya vitu hivyo nilivyovitaja bado unaweza kutengeneza Website Bila Tatizo lolote.

Ni muhimu kujua codes (HTML na CSS) kama unataka kuwa mtaalamu zaidi katika Website Design.

Unaweza kujifunza HTML na CSS kwa urahisi zaidi kupitia Viungo vilivyopo hapa chini

 

HTML

https://www.w3schools.com/html/

https://www.tutorialspoint.com/html/index.htm

 

CSS

https://www.w3schools.com/css/default.asp

https://www.tutorialspoint.com/css/index.htm

 

Kama una swali lolote unaweza kuuliza hapo chini.

Comments

Popular posts from this blog

Kwa Nini Ni Lazima Ujifunze Microsoft Excel-Sababu 5 za Msingi

Microsoft Excel ni Program ya kimahesabu inayotumika kuhifadhi data katika muundo wa nambari, maneno, grafu na chati. Microsoft Excel inatumika katika makampuni biashara na katika taasisi mbalimbali. Pia watu binafsi hutumia program hii kwa matumizi mbambali. Kuna sababu tano za msingi za wewe kujifunza   Microsoft Excel. 1.Kuongeza ufanisi katika kazi. Program ya microsoft excel inakusaidia kuongeza ufanisi katika kazi unazofanya kutokana na uwezo wake wa kurahisisha kazi na kuokoa muda. Mfano kama ulitakiwa kutengeneza ripoti 100 kwa njia ya mkono ungeweza  kutumia hata siku nzima kuandaa tu, lakini kupitia Microsoft excel unaweza kukamilisha kazi hiyo ndani ya saa 1 au masaa mawili tu. 2.Kutunza taarifa binafsi. Unaweza kutumia program ya Microsoft Excel  kutunza taarifa zako binafsi kama vile orodha ya vitu, bajeti yako binafsi au kufanyia mahesabu muhimu ya manunuzi / matumizi unayoyafanya. 3.Kufanya mahesabu ya kibiashara. Program ya Microsoft excel ina umu...